Monday, September 25, 2023
HomeNewsCOVID 19 UpdatesWatu wawili zaidi Waaga kutokana na CoronaVirus

Watu wawili zaidi Waaga kutokana na CoronaVirus

Idadi ya watu walioambukizwa virusi vya corona nchini imetimia 110, waziri wa Afya Mutahi Kagwe ametangaza. Akizungumza katika mkutano na wanahabari Alhamisi hii, Kagwe alisema kuwa watu wengine wawili wamepoteza maisha yao kutokana na maambukizi ya virusi hivyo.

Hivyo basi idadi ya waliofariki kutokana na virusi hivyo nchini imefikia watatu. Kagwe pia amepiga marufuku safari za kuelekea mashambani akionya Wakenya kwamba huenda wakaeneza maambukizi ya virusi hivyo kwa kiwango kikubwa.

Waziri Kagwe pia amechukua nafasi hiyo kuwaponda wakenya wanaokejeli wakenya wawili Brenda na Brian waliotangazwa kuwa walipona virusi hivyo.

Kamadi Amatahttps://mtaaniradio.or.ke
I am a digital content creator with niche in Health, politics, and Human Interest Features.
RELATED ARTICLES

Most Popular

Recent Comments

Education Template

Facebook